• Toll Free: 0800110088
  • Box: 2932, Sinde Area - Mbeya Tanzania

Ziara ya Bodi ya Wakurugenzi

Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya , leo tarehe 23/11/2023 imefanya ziara ya kutembelea miradi ya maji inayotekelezwa na Mamlaka. Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bi.Edna Mwaigomole amesema lengo la ziara hiyo ni kujionea hatua za utekelezaji wa miradi na kiwango cha ubora wa kiufundi kulinganisha na usanifu ili kukidhi vigezo vya kutoa huduma ya majisafi kwa wananchi.

Kilele cha Wiki ya Huduma kwa Mteja

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya imekabidhi mashuka 100 yenye gharama ya sh. 2,400,000 kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya, ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa mteja

Utiajia Saini Mkataba wa kutekeleza mradi wa Kiwira

Waziri wa Maji Jumaa Hamidu Aweso, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson, Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi pamoja na Mkuu wa Mkoa Mbeya Juma Zuberi Homera wakishuhudia zoezi la utiwaji saini mradi wa maji kutoka chanzo cha mto Kiwira

Uzinduzi wa Mradi wa Maji Shongo - Mbalizi

Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akizindua mradi mkubwa wa maji Shongo Mbalizi jijini Mbeya.

Mradi wa Kiwira

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi Mbeya (Kushoto) wakati wa hafla ya kutia saini Mkataba wa kuanza kazi ya kutekeleza mradi wa maji kutoka mto Kiwira

Maelezo ya Mradi

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera akipokea maelezo ya Mradi wa Maji Nzovwe-Isyesye alipotembelea miradi inayotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi Mbeya

Kutembelea wateja wakubwa

Mamlaka imetembelea Jeshi la Magereza ili kuwapa Elimu juu ya huduma za maji ikiwa ni pamoja na matumizi ya maji, bei za maji na jinsi ya kufanya malipo.

Kutunza vyanzo vya Maji

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi Mbeya akipanda miti katika maadhimisho ya Wiki ya Maji.

Usafi wa Mazingira

Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka wakifanya usafi wa Mazingira katika Wiki ya Maji.

Kutunza Vyanzo vya Maji

Maji ni Uhai, tunza vyanzo vya Maji

KARIBU MAMLAKA YA MAJISAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MBEYA

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (Mbeya UWSA) ni miongoni mwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanzania Bara. Mamlaka ilianzishwa mwaka 1998 kwa Sheria Na. 8 ya 'Water Works Act Cap 272' ya mwaka 1997, iliyofanyiwa marekebisho na Sheria Na.12 ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2009. Mamlaka ya Majisafi Mbeya imepatiwa daraja "A".

Mamlaka ya daraja "A" inawajibika kugharamia shughuli za uendeshaji, matengenezo, mishahara na kuchangia asilimia 15% ya mapato yake kwenye shughuli za maendeleo. Mamlaka ina dhamana ya kutoa huduma bora ya majisafi pamoja na usafi wa mazingira kwa wakazi waishio Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi iliyopo Kusini Magharibi mwa Tanzania. Miji hii inakadiriwa kuwa na wakazi wapatao 630,000 (Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022).

DIRA (VISION)

Kuwa mamlaka bora kwa kutoa huduma bora na endelevu ya majisafi na usafi wa mazingira ifikapo 2025.

DHIMA (MISSION)

Kutoa huduma bora na endelevu ya majisafi na usafi wa mazingira kwa wakazi wa Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi kwa bei himilivu.

KAULIMBIU (SLOGAN)

'Maji ni Uhai'

MISINGI YA UTENDAJI (CORE VALUES)
  • Wateja Kwanza
  • Watumishi ni Rasilimali namba moja ya Mamlaka
  • Kuwajibika kwa jamii inayotuzunguka
  • Nidhamu katika matumizi ya Fedha
  • Watumishi kufanyakazi kwa pamoja na kujituma.
  • Wafanyakazi kuhimizwa kujifunza na kubadilishana maarifa.
MACHAPISHO NA FOMU

MKURUGENZI MTENDAJI CPA. Gilbert Kayange


KURIPOTI MIVUJO NA WIZI WA MAJI

Ili kuripot mvujo wa maji (Mfano: bomba kupasuka n.k), kuripoti wizi wa maji au uharibifu wowote wa miundombinu ya maji, tafadhali piga simu ya Ofisi namba: 0800110088 bure.

GALLERY


Bonyeza hapa kwa picha zaidi

Habari Mpya

Matukio Kwa Picha

ZOEZI LA UPANDAJI MITI CHANZO CHA MWATEZI

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya kwa kushirikiana na Kampuni ya TBL leo tarehe 20/03/2024 wamepanda miti katika chanzo cha maji cha Mwatezi kilichopo Uyole Jiji Mbeya kwa lengo la kuhimiza utunzaji wa mazingira. Katika kuadhimisha Wiki ya Maji, kampuni ya TBL imetoa miti 300 na kushiriki kupanda katika chanzo cha maji, ili kuunga mkono jitihada za serikali za kuhakikisha huduma ya maji inakuwa bora na endelevu katika jamii kwa kutunza vyanzo vya maji

MADIWANI WANAWAKE VITI MAALUMU MBEYA WATEMBELEA MIRADI YA MAJI

Madiwani Wanawake viti maalumu Jiji la Mbeya na Mbeya Vijijini, waipongeza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya, kwa kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa miradi ya Maji Jijini Mbeya na Mji wa Mbalizi. Aidha, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mbeya UWSA, Mhandisi Barnabas Konga, amewaomba madiwani hao kushirikiana na Mamlaka katika kutoa elimu ya utunzaji wa vyanzo na miundombinu ya maji ili kuboresha huduma ya maji na kutatua changamoto ya maji kwa wananchi.

WATUMISHI WAKABIDHIWA PIKIPIKI TANO

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MBEYA - UWSA, Mhandisi Barnabas Konga leo tarehe 18/03/2024 amekabidhi pikipiki tano(5) kwa Watumishi wa vitengo ndani ya Mamlaka ili kurahisisha utendaji kazi na kuwafikia wateja kwa haraka. Akikabidhi pikipiki hizo, Mhandisi Konga amewasihi watumishi hao kutumia vyombo hivyo kwa ungalifu na kuwafikia na kutatua changamoto za wateja kwa wakati.